Rais Dkt.Mwinyi aipongeza Stanbic Bank kwa kuwa mshirika wa maendeleo Zanzibar

ZANZIBAR-Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mhe. Dkt. Hussein Mwinyi ameipongeza Benki ya Stanbic kwa kuwa mshirika wa maendeleo Zanzibar na kwa kuleta suluhisho za kifedha zenye manufaa kwa nchi na wananchi wa Zanzibar katika miradi ya kimkakati.
Rais Dkt.amesema hayo alipokutana na Afisa Mtendaji Mkuu wa Benki ya Stanbic Tanzania, Bw. Manzi Rwegasira, Ikulu Zanzibar mapema leo.
Naye Bw.Manzi ameihakikishia Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar juu ya utayari wa Benki ya Stanbic kuendelea kushirikiana nayo katika kufanikisha miradi ya maendeleo.

Ameeleza kuwa Benki ya Stanbic, kufuatia utiliaji wa saini wa mkataba wa leo kwa kushirikiana na Benki ya Watu wa Zanzibar (PBZ), tayari itakuwa zimeshatoa jumla ya mkopo wa pamoja shilingi bilioni 185 kati ya bilioni 500 zinazohitajika kwa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar ili kufadhili miradi ya maendeleo.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news