Rais Dkt.Mwinyi akabidhi Sadaka ya Futari kwa makundi maalum Zanzibar

ZANZIBAR-Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dkt.Hussein Ali Mwinyi amekabidhi Sadaka ya Futari kwa wananchi mbalimbali wa Mkoa wa Mjini Magharibi.
Makabidhiano hayo yamefanyika Viwanja vya Mapinduzi Square huko Michenzani ambapo wananchi mbalimbali waliojitokeza kupokea sadaka hiyo.
Akizungumza katika hafla hiyo, Rais Dkt. Mwinyi amefahamisha kuwa,sadaka hiyo imetolewa na mfadhili ndugu Jaffar aliyemkabidhi Dkt.Mwinyi ili kuwagawia wananchi.

Rais amemshukuru hfadhili huyo na wananchi waliojitokeza kuipokea.

Wakati huohuo Rais Dkt.Mwinyi amekabidhi sadaka hiyo ya bidhaa za chakula kwa wakuu wa Wilaya za Mkoa wa Mjini Magharibi ili kuendelea na ugawaji kwa wananchi katika wilaya wanazoziongoza.
Naye Mkuu wa Mkoa wa Mjini Magharibi, Idrissa Kitwana amemshukuru Dkt.Mwinyi kwa kuendeleza utaratibu huo kila mwaka kwa Makundi Maalum ya Watu wenye Ulemavu, Yatima, Wajane na Wanaoishi katika Mazingira Magumu.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news