Rais Dkt.Samia ateua viongozi na kuwapangia mabalozi vituo

ZANZIBAR-Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan amefanya uteuzi wa viongozi mbalimbali na kuwapangia vituo mabalozi.
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Katibu Mkuu Kiongozi Balozi Dkt. Moses Kusiluka, uteuzi na kupangiwa vituo Mabalozi ni kama ifuatavyo:-

i.Bi. Rachel Stephen Kasanda ameteuliwa kuwa Mkuu wa Wilaya ya Masasi. Bi.Kasanda anachukua nafasi ya Bw. Lauteri John Kanoni ambaye uteuzi wakeumetenguliwa;

ii.Prof. Jafari Ramadhani Kideghesho ameteuliwa kuwa Mwenyekiti wa Bodi yaWadhamini ya Mfuko wa Uhifadhi wa Wanyamapori Tanzania;

iii.CPA.Ashraph Yusuph Abdulkarim ameteuliwa kuwa Meneja Mkuu wa Shirika la Masoko Kariakoo

;iv.Balozi Hamad Khamis Hamad amepangiwa kuwa Balozi wa Tanzania nchini Msumbiji;na

V.Balozi Mobhare Holmes Matinyi amepangiwa kuwa Balozi wa Tanzania nchini Sweden.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news