Rais Wallace Karia afunguka Derby ya Kariakoo kuahirishwa

DAR-Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Wallace amejibu tuhuma wanazoshushiwa bodi ya Ligi kufuatia uamuzi wa kuahirisha mchezo wa Kariakoo Derby uliopaswa kuchezwa Machi 8, 2025.
Akizungumza katika mahojiano na Wasafi Fm katika kipindi cha Jana na Leo, Rais Karia amedai kuwa bodi iachwe ifanye kazi yake.

Pia,amebainisha kuwa,walisimamia na watasimamia kanuni na sheria inavyopaswa, lakini kwa wanaosema bodi hiyo itenguliwe nao wanapaswa kujihoji kama uongozi wao upo sawa.

"Taratibu tuziache zifuatwe, Lakini huwezi kusema bodi ijiuzulu. Hata wanaosema wawaambie na viongozi wao, hawastahili kujiuzulu?.

"Vitu vingine vinafanyika kitoto,kama watu wamechoka kucheza mpira basi wakaendelee na sinema zao.

Mbali na hayo amesema kuwa, “Kuna siku tulipokea barua kutoka CAF wakihitaji waamuzi wetu wawili kwenda kuchezesha michuano ya Kimataifa.

“Wakati barua ile imekuja ofisini kuhitaji wale waamuzi kulikuwa na changamoto. Kwani mojawapo ya wale waamuzi ambaye ni Ahmed Arajiga alikuwa amefungiwa na kamati ya masaa 72.

“Ilikuwa ngumu sana kwangu, maana CAF wamemtaka mwamuzi, halafu huku kwetu kamati imemfungia, lakini nikafanya maamuzi.

“Nilifanya maamuzi nikawaambia hawa waamuzi waruhusiwe waende,walienda wote wawili,lakini bahati mbaya mmoja ndio alifuzu ambaye ni Ahmed Arajiga.

“Yalikuwa maamuzi magumu ila sikuwa na namna na Ahmed Arajiga alienda kuwakilisha Tanzania vema sana.Hata mechi aliyochezesha alichezesha vizuri sana”

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news