Singida Black Stars kuzindua uwanja wake wa Airtel Stadium

SINGIDA-Klabu ya Singida Black Stars imetangaza rasmi kuzindua uwanja wao mpya wa kisasa unaoitwa Airtel Stadium uliopo katika eneo la Mtipa mkoani Singida.
Uzinduzi wa uwanja huo mpya wa klabu hiyo utafanyika Machi 24, 2025 mkoani Singida, ambapo watacheza mchezo wa kirafiki dhidi ya Yanga SC.

"Airtel Stadium ni sehemu ya dhamira ya Singida Black Stars ya kuwekeza katika maendeleo ya michezo kwa kutoa mazingira bora kwa wachezaji, mashabiki na jamii kwa ujumla.

"Uwanja huu umejengwa kwa viwango vya kimataifa na unatarajiwa kuwa kitovu cha mashindano makubwa ya kitaifa na kimataifa," imeeleza taarifa ya klabu hiyo.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news