Tuendelee kuiombea nchi idumu katika amani kwa maendeleo zaidi-Rais Dkt.Mwinyi

ZANZIBAR-Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi,Dkt.Hussein Ali Mwinyi amewahimiza wananchi kuendelea kuiombea nchi amani ili maendeleo zaidi yapatikane.
Rais Dkt. Mwinyi ameyasema hayo Machi 21,2025 alipojumuika na waumini wa Dini ya Kiislamu katika Sala ya Ijumaa Msikiti wa Weles Kikwajuni Wilaya ya Mjini, Mkoa wa Mjini Magharibi.
Aidha,Rais Dkt.Mwinyi amewasisitiza waumini na wananchi kuweka azma ya kuendeleza amani iliyopo hususani wakati huu wa kuelekea Uchaguzi Mkuu wa mwezi Oktoba.

Amefahamisha kuwa,kipindi cha miaka mitano ya Awamu ya Nane mambo mengi ya maendeleo yamefanyika katika nyanja zote kutokana na nchi kuwa na amani,hivyo kuna wajibu wa kudumishwa.
Halikadhalika,Rais Dkt.Mwinyi amewasihi waumini hao kuongeza bidii katika ibada katika kumi la Mwisho la Mwezi wa Ramadhani.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news