VIDEO:Wanawake wa PSSSF wapeleka tabasamu kwa wanafunzi na shule Dodoma

DODOMA-Kuelekea kilele cha Siku ya Wanawake Duniani, Mfuko wa Hifadhi ya Jamii kwa Watumishi wa Umma (PSSSF) umekabidhi msaada wa fedha kwa ajili ya kuboresha miundombinu ya shule na usambazaji wa taulo za kike kwa wanafunzi wa kike wenye uhitaji.
Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Bi. Rosemary Senyamule amewapongeza wanawake wa PSSSF kwa mchango huo katika kuboresha mazingira ya elimu hapa nchini na kuwapunguzia adha watoto wa kike kutembea umbali mrefu kufuata shule jambo ambalo linawaweka katika hatari mbalimbali.

"Mmechagua njia nzuri ya kusherehekea siku ya wanawake duniani ambayo inaacha sura isiyofutika, mngeweza pesa yenu kuishia kula na kufurahi kwa namna yenu lakini mmeamua kutunza kumbukumbu kubwa katika historia ya shule hii;

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news