Vijana wa Dodoma wahimizwa kujikomboa dhidi ya dawa za kulevya

DODOMA-Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Mhe. Rosemary Senyamule amewataka vijana wa mkoa huo kuwa mstari wa mbele katika mapambano dhidi ya dawa za kulevya.
Akizungumza katika kongamano lililoandaliwa na Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya (DCEA) kwa kushirikiana na Taasisi ya Taifa Forum, Mhe. Senyamule alisisitiza kuwa vijana wana jukumu kubwa katika kutokomeza tatizo hili.
Kongamano hilo, lililohudhuriwa na vijana zaidi ya 1,500 kutoka vyuo mbalimbali vya Dodoma, vikiwemo Chuo cha Mipango, CBE, VETA, pamoja na waraibu walio kwenye matibabu, lililenga kutoa elimu na kuhamasisha vijana kushiriki kikamilifu katika vita dhidi ya dawa za kulevya.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news