ARUSHA-Kufuatia Kilele cha Maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani yanayotegemea kufanyika Kitaifa jijini Arusha tarehe 8 Machi, 2025 yaliyotanguliwa na maonesho na utoaji wa Elimu kwa Umma katika Viunga vya Uwanja wa Shekhe Amri Abeid Jijini humo, Wananchi wanaotoka katika maeneo ya Mkoa wa Arusha na mikoa jirani wamefurika katika banda la Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu).

Maeneo mengine ni pamoja na elimu ya mifugo, kilimo na Uvuvi kupitia programu ya Kuendeleza ya kilimo na uvuvi (AFDP) pamoja na Program ya Kuendeleza Sekta ya Kilimo Awamu ya Pili (ASDP II).
Watalaam hao wanawake kutoka katika Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu) wameonekana wakitoa elimu hiyo kwa makundi mbali mbali ya wanawake wasichana na vijana wa rika tofauti tarehe 07 Machi 2025 na kuendelea.
Maadhimisho hayo yanatanguliwa na Kaulimbiu inayosema "Wanawake na Wasichana 2025: Tuimarishe Haki, Usawa na Uwezeshaji".