Waziri Mkuu aridhishwa na maandalizi kuelekea kuwashwa kwa Mwenge wa Uhuru

PWANI-Waziri Mkuu Kassim Majaliwa amesema ameridhishwa na hatua za maandalizi kuelekea sherehe za kuwashwa kwa Mwenge wa Uhuru ambao utazunguka katika Mikoa 31 na Halmashauri 195 nchini.
Amesema hayo Machi 30, 2025 baada ya kukagua maandalizi hayo katika uwanja wa uwanja wa Shirika la Elimu Kibaha Mkoani Pwani. Mgeni rasmi katika sherehe hizo zitakazofanyika Aprili 02, 2025 atakuwa ni Makamu wa Rais Dkt. Philip Isdor Mpango.
Akizungumza baada ya kukagua maandalizi hayo Mheshimiwa Majaliwa ametoa wito kwa waratibu wote wa Sherehe hizo kuhakikisha wanakamilisha haraka maeneo machache yaliyobaki.

"Nimeridhishwa na maandalizi yaliyofanyika, mmefanya kazi kubwa hadi kufikia hatua hii, tuhakikishe sehemu ndogo zilizobaki tunazikamilisha kwa wakati."
Naye Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Kazi Vijana Ajira na Wenye Ulemavu Ridhiwani Kikwete amesema maandalizi hayo yamefikia asilimia 96 na maeneo machache yaliyobaki yatakamilishwa ndani ya muda mfupi.

Awali, akitoa salamu za Mkoa wa Pwani, Mkuu wa Mkoa huo Abubakar Kunenge amesema kuwa wamejipanga vyema kuhakikisha sherehe hizo zinafanyika kwa mafanikio makubwa.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news