Zanzibar itaongeza idadi ya watalii kutoka barani Asia-Rais Dkt.Mwinyi

ZANZIBAR-Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dkt.Hussein Ali Mwinyi amesema, Zanzibar inafanya kila juhudi kuhakikisha inaongeza idadi ya watalii kutoka barani Asia.
Dkt.Mwinyi amesema hayo leo Machi Mosi,2025 alipozungumza na waigizaji na watengenezaji wa filamu kutoka India waliofika Ikulu Zanzibar.
Aidha, Rais Dkt.Mwinyi ameeleza kuwa Zanzibar iko tayari kushirikiana na India kutangaza Vivutio vya Utalii nchini humo na kuwataka kuwa Mabalozi Wazuri watakapokuwa nchini kwao.

Halikadhalika, Rais Dkt.Mwinyi amesema Uzoefu na Umahiri wa Waigizaji na Watengezaji wa Filamu wa India ni fursa Muhimu inayoweza kutumika kuitangaza Zanzibar ili Kuongeza Watalii kutoka India.

Vilevile Rais Dkt.Mwinyi amewapongeza kwa kuja nchini na Serikali ipo tayari kushirikiana nao kikamilifu kuitangaza Sekta ya Utalii ya Zanzibar.
Naye Mkuu wa timu hiyo ya Waigizaji kutoka Taasisi ya JIO CREATIVE LABS Aditya Bhat amesema ziara yao imefungua fursa za Ushirikiano na wako tayari kuvitangaza Vivutio vyà Utalii vya Zanzibar nchini India kupitia fani zao.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news