Dkt.Natu El-Maamry Mwamba afanya mazungumzo na Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje wa Sweden

WASHINGTON-Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na Mlipaji Mkuu wa Serikali, Dkt. Natu El-maamry Mwamba, amekutana na kufanya mazungumzo na Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje wa Sweden, Bi. Diana Janse kando ya Mikutano ya Majira ya Kipupwe, ya Shirika la Fedha la Kimataifa (IMF) na Benki ya Dunia ya mwaka 2025, inayofanyika jijini Washington D.C nchini Marekani.
Katika mazungumzo yao yaliyofanyika katika Ubalozi wa Marekani, jijini Washington, Dkt. Mwamba na mgeni wake, wamejadiliana masuala kadhaa ya kuimarisha zaidi ushirikiano wa kiuchumi kati ya Tanzania na Sweden, ikiwemo utekelezaji wa miradi mbalimbali ya kimkakati inayotekelezwa na Serikali na pia kuendeleza mashirikiano ya kibiashara na kiuchumi kati ya nchi hizo mbili.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news