Meneja RUWASA wilayani Kakonko,wenzake hatiani kwa makosa ya rushwa na uhujumu uchumi

KIGOMA-Aprili 8, 2025, Mahakama ya Wilaya ya Kakonko mkoani Kigoma imewatia hatiani Meneja wa Wakala wa Maji na Usafi wa Mazingira Vijijini (RUWASA) Wilaya ya Kakonko, Mhandisi Benjamin Mjuni Brighton (37) na wenzake wawili.
Ni katika Shauri la Uhujumu Uchumi namba 2735/2025 mbele ya Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Mahakama ya Wilaya ya Kakonko, Mheshimiwa Ambilike Japhet Kyamba na Wakili wa Serikali kutoka Ofisi ya TAKUKURU Mkoa wa Kigoma,Bw. Jackson George Lyimo,

Wengine waliotiwa hatiani ni Fundi Sanifu wa RUWASA Wilaya ya Kakonko,Bi. Faraja Charles Kalokola (27) na Mkurugenzi wa Kampuni ya Chiganda Construction Limited Bw. Johansen Martine Muganyizi (46).

Kwa pamoja walishtakiwa kwa makosa ya matumizi ya nyaraka kwa lengo la kumdanganya mwajiri,kujipatia manufaa, ubadhirifu na ufujaji.

Vilevile,matumizi mabaya ya mamlaka pamoja na ushawishi kinyume na vifungu vya 22, 23 (1), 28 (1), 31 na 33 vyote vya Sheria ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa Sura namba 329 Marejeo ya mwaka 2022 ikisomwa pamoja na aya ya 21 ya jedwali la kwanza, kifungu cha 57(1) na kifungu 60(2) vya Sheria ya Udhibiti wa Makosa ya Uhujumu Uchumi na Uhalifu wa Kupangwa Sura namba 200 Marejeo ya Mwaka 2022.

Washtakiwa wamehukumiwa kulipa faini ya sh. 4,000,000/= na kurejesha sh. 53,922,660/= zilizofanyiwa ubadhirifu.

International news

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post