Rais Dkt.Mwinyi aipongeza Simba SC kwa ushindi dhidi ya Stellenbosch FC

ZANZIBAR-Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi,Dkt. Hussein Ali Mwinyi amewapongeza wachezaji wa timu ya Simba kwa ushindi walioupata katika mashindano ya Kombe la Shirikisho Barani Afrika, katika mchezo wa awali wa Nusu Fainali dhidi ya timu ya Stellenbosch Football Club ya Afrika Kusini.
Aidha, RaiRaist. Mwinyi ametoa pongezi hizo akiwa katika makazi yake ya Ikulu Ndogo Migombani, Zanzibar, akifuatilia mchezo huo uliochezwa katika Uwanja wa New Amaan Complex, Wilaya ya Mjini, Mkoa wa Mjini Magharibi tarehe 20 Aprili 2025.

Halikadhalika, Rais Dkt.Mwinyi ameipongeza timu ya Simba kwa kuuchagua Uwanja wa New Amaan Complex kuwa uwanja wao wa nyumbani na kueleza kuwa Serikali imefarijika na hatua hiyo, huku akiahidi kuendelea kuimarisha viwanja mbalimbali hapa Zanzibar.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news