Rais Dkt.Samia ateua viongozi mbalimbali wa taasisi za umma

DAR-Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan amefanya uteuzi wa viongozi mbalimbali wa taasisi za umma, kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi Dkt. Moses Kusiluka.
Prof. John Kondoro ameteuliwa kuwa Mwenyekiti wa Kamisheni ya Tume ya Taifa ya Sayansi na Teknolojia (COSTECH), kuchukua nafasi ya Prof. Makenya Maboko ambaye amemaliza muda wake.

Prof. Emanue Mjema ameteuliwa kuendelea na kipindi cha pili kama Mwenyekiti wa Baraza la Uongozi la Chuo cha Usimamizi wa Fedha (IFM).

Mhandisi Mwanasha Tumbo ameteuliwa kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC), akichukua nafasi ya Prof. Esnat Chaggu aliyemaliza muda wake.

IGP Mstaafu Balozi Simon Sirro ameteuliwa kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Shirika la Madini la Taifa (STAMICO), nafasi iliyokuwa ikishikiliwa na Meja Jenerali Mstaafu Michael Isamuhyo.

Rosemary Silaa ameteuliwa kuendelea na kipindi cha pili kama Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini ya Bohari ya Dawa (MSD).

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news