ARUSHA-Tanzania imeendelea kushikilia rekodi ya ubora duniani katika viwango vya usimamizi wa hali ya juu vya usalama mitandaoni.

Amesema, kwa mujibu wa ripoti ya Usalama Mtandaoni (Global Cybersecurity Index (GCI) ya mwaka 2024 iliyotolewa na Shirika la Mawasiliano Duniani (ITU),Tanzania imewekwa katika Kundi la 1 (Tier 1), ambayo ni ngazi ya juu zaidi duniani kwa ubora wa usalama mtandaoni. "Duniani kote ni nchi 46 tu zenye hadhi hii."

Hatua hiyo amesema, imetokana na vipimo vya GCI kubaini Tanzania imepiga hatua kubwa katika masuala ya kisheria kuhusu usalama mtandaoni.
Pia, ripoti hiyo ilibaini Tanzania imepiga hatua kubwa kwa upande wa mikakati na mipango ya kiufundi, kiutawala, uendeshaji wa mifumo, kujenga uwezo na ushirikiano katika masuala yanayohusu usalama mtandaoni.

Pia, amesema jukwaa hilo la siku mbili linaongozwa na kaulimbiu isemayo, "Kuimarisha Uimara na Kukabiliana na Vitisho Katika Uchumi wa Kidijitali".
Vilevile, Dkt.Mwasaga amesema, jukwaa hilo linajumuisha mijadala ya wataalamu, warsha za kiufundi, mijadala ya kisera, fursa za kujenga mtandao wa ushirikiano, pamoja na mafunzo ya vitendo yenye lengo la kuimarisha uimara wa Tanzania dhidi ya matishio ya usalama mtandaoni.
Dkt.Mwasaga amesema, miongoni mwa mada zitakazojadiliwa ni kuhusu namna ya kuimarisha ushirikiano kwa ajili ya mtandao endelevu na jumuishi, kuendeleza uimara wa sekta muhimu.
Mada nyingine, Dkt.Mwasaga amesema, itaangazia juu ya namna ya kulinda mtandao katika enzi ya teknolojia zinazoibuka na nyingine ni namna ya kutumia mtandao kama injini ya ukuaji wa uchumi.

"Nguzo ya pili inahusiana na usalama wa mtandao, ulinzi wa taarifa binafsi, na ulinzi wa watumiaji katika uchumi wa kidijitali."
Nguzo nyingine ni huduma za mawasiliano ya kidijitali,uchumi wa kidijitali, utafiti wa kidijitali,ubunifu na ujasiriamali.

Miongoni mwa maazimio hayo, Dkt.Mwasaga amesema yalikuwa ni;
a) Kuongeza uelewa kwa umma kuhusu Sheria ya Ulinzi wa Taarifa Binafsi
b) Kuhamasisha ushiriki wa wataalamu wa usalama wa mtandao katika mabadiliko ya kidijitali
c) Kusaidia ubunifu wa ndani na suluhisho katika usalama wa mtandao
d) Kupitia sheria za usalama wa mtandao ili kujumuisha wataalamu wa ndani
e) Kutambua wataalamu waliothibitishwa na Tume ya TEHAMA
f) Kuwekeza zaidi kwenye kukuza uwezo wa ndani katika usalama wa mtandao
g) Kukuza makampuni ya ndani yanayotoa huduma za usalama wa mtandao
h) Kuweka suluhisho katika kitambulisho cha kidijitali.
i) Kuanzisha bima ya usalama wa mtandao ili kupunguza hasara za kifedha
j) Kuhamasisha ushiriki wa wanawake katika elimu ya usalama wa mtandao
k) Kutambua usalama wa mtandao kama kichocheo cha ukuaji wa uchumi
l) Kuwakutanisha wadau muhimu katika mijadala ya baadaye kuhusu mtandao
Changamoto
Dkt.Mwasaga akizungumzia kuhusu changamoto za Kimataifa za kiusalama mtandaoni amesema, kwa mujibu wa ITU, changamoto kubwa ni kuongezeka kwa programu hasidi (ransomware).

Dkt.Mwasaga amesema, nyingine ni ukiukwaji wa faragha ambapo Ulaya pekee ilitoza faini zaidi ya Euro bilioni 1.9 mwaka 2023.
Pia, kuna suala la gharama kubwa katika biashara ambapo wastani wa gharama ya wizi wa data ilikuwa dola za kimarekani milioni 4.45 mwaka 2023 ikiwemo hitilafu za mfumo zinazoathiri huduma na minyororo ya usambazaji.
Amesema,kadri uhalifu wa kimtandao unavyozidi kuongezeka, ni muhimu kwa biashara, taasisi za serikali, na watu binafsi kuchukua hatua za mapema za kujilinda dhidi ya vitisho hivyo na kulinda taarifa nyeti pamoja na miundombinu yake muhimu.
Jukwaa hili linaendana na Dira ya Tanzania ya kuwa na Uchumi wa Kidijitali ulio salama na wenye mafanikio.