Tuzo za Samia Kalamu Awards 2025 zahamishiwa Dar

DAR-Chama cha Waandishi wa Habari Wanawake Tanzania (TAMWA), kwa kushirikiana na Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) kinapenda kuwatangazia washiriki,wadau wa sekta ya habari na umma kwa ujumla kuhusu mabadiliko ya tarehe na mahali pa kufanyika kwa hafla ya utoaji wa Tuzo za Uandishi wa Habari za Maendeleo-Samia Kalamu Awards 2025.

Hafla hiyo, ambayo awali ilikuwa imepangwa kufanyika tarehe 29 Aprili 2025 katikaUkumbi wa Mabele,Mabeyo Complex, jijini Dodoma, sasa itafanyika tarehe 5 Mei 2025 jijini Dar es Salaam katika ukumbi utakaotangazwa hivi karibuni.

Mabadiliko haya yanatokana na sababu za kiutendaji zisizoweza kuepukika. 

Aidha, waalikwa wote watatumiwa mwaliko mpya wenye maelezo kamili kuhusu eneo na ratibaya tukio hilo.

Mgeni Rasmi katika tukio hili anatarajiwa kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan.

Tunaomba radhi kwa usumbufu uliojitokeza kutokana na mabadiliko haya na tunawashauri washiriki wote kuendelea na maandalizi ya kushiriki kwenye hafla hii adhimu inayolenga kutambua na kuthamini mchango mkubwa wa wanahabari katika maendeleo ya taifa letu.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news